Kitubio/Maungamo
Sakramenti ya Kitubio: Kitubio, pia kinacho julikana kama maungamo, ni sakramenti muhimu ambapo waumini wanatubu dhambi zao na kupokea msamaha kutoka kwa Mungu kupitia kwa kuhani. Parokia yetu ina ratiba maalum za kitubio ambapo waumini wanaweza kumwendea kuhani kwa ajili ya kitubio.

Maandalizi ya Kitubio: Tunatoa mafundisho na maandalizi kwa waumini, hasa watoto na vijana, ili kuhakikisha wanajua umuhimu wa sakramenti ya kitubio na jinsi ya kujiandaa vizuri kwa ajili ya kitubio.
