Jumuiya Ndogo Ndogo na Mitaa
Parokia ya Mt. Francis Xavier Nyakahoja imeundwa na jumuiya ndogo ndogo 32 na mitaa 11. Kila jumuiya na mtaa una viongozi wake ambao wanasaidia katika kuratibu shughuli za kiroho na kijamii katika maeneo yao.

Shughuli za Kijamii
Parokia yetu inahusika katika shughuli mbalimbali za kijamii kama vile misaada kwa wasiojiweza, elimu, na afya, ikilenga kuboresha maisha ya watu wote katika jamii. Tunajitahidi kuhakikisha kuwa waumini wetu wanapata huduma bora za kiroho ambazo zitawasaidia kuimarisha imani yao na kuishi maisha ya Kikristo yenye mafanikio. Pia, tunatoa huduma za ushauri wa kiroho kwa wale wanao pitia changamoto za maisha na tunasaidia familia kujenga mahusiano bora na yenye afya kwa mujibu wa mafundisho ya Kikristo.

