Parokia inaendelea kuwahimiza vijana na familia kushiriki katika semina, mafungo, makongamano na vipindi vya malezi ya kiroho vinavyosaidia kukua katika maisha ya imani na maadili. Vijana ni nguvu ya Kanisa la leo na la kesho; familia ni shule ya kwanza ya imani, upendo na maadili mema.

Kwa pamoja, vijana na wazazi wanaalikwa kuwa mfano wa uwajibikaji, mshikamano na uaminifu kwa Mungu. Kupitia mafundisho, sala na huduma za pamoja, parokia inaendelea kujenga kizazi chenye matumaini, nidhamu na moyo wa kujitoa.

Karibu tushirikiane kuijenga parokia yetu kwa moyo mmoja na kwa nia ya kumtukuza Mungu katika kila hatua ya maisha.
